BONGOSOUL
Tupo Kwenye Kila Trend · Tanzania 🇹🇿
EST. 2024 🇹🇿
Nutrition & Diet

Mpangilio wa sahani Kwa Mgonjwa wa kisukari (Diabetic plate Guide)

Mpangilio wa sahani Kwa Mgonjwa wa kisukari (Diabetic plate Guide) ni njia rahisi ya kumfundisha mgonjwa wa kisukari jinsi ya kupanga chakula kwenye sahani ili kudhibiti sukari ya damu.

Mpangilio wa sahani Kwa Mgonjwa wa kisukari (Diabetic plate Guide)

Mpangilio wa sahani Kwa Mgonjwa wa kisukari (Diabetic plate Guide) ni njia rahisi ya kumfundisha mgonjwa wa kisukari jinsi ya kupanga chakula kwenye sahani ili kudhibiti sukari ya damu.

  1. Gawanya sahani katika sehemu 3

Nusu ya sahani (1/2) – Mboga
Weka mboga nyingi zisizo na wanga mwingi. Mfano: mchicha, kabichi, matembele, broccoli, spinach, biringanya.

Robo ya sahani (1/4) – Protini
Hii ni chakula kinachojenga mwili. Mfano: samaki, kuku, nyama isiyo na mafuta mengi, maharage, dengu, mayai.

Robo ya sahani (1/4) – Wanga (carbohydrates)
Weka kiasi kidogo cha wanga kama: ugali, wali, viazi, ndizi za kupika, mkate, wali wa kahawia.

  1. Ongeza tunda kidogo pembeni
    Chagua tunda moja kwa kiasi, mfano: apple, chungwa, papai kidogo, tikiti maji. Epuka kula matunda mengi kwa wakati mmoja.

  2. Tumia maji au vinywaji visivyo na sukari
    Epuka soda, juice zenye sukari nyingi na chai yenye sukari nyingi.

  3. Epuka vyakula vya kukaanga sana
    Chagua vyakula vilivyochemshwa.

  4. Kula kwa muda unaofanana kila siku
    Hii husaidia kudhibiti sukari ya damu vizuri.

Mfano wa sahani kwa mazingira ya Tanzania
• Nusu sahani: mchicha na kabichi
• Robo sahani: samaki, kipande cha kuku (paja)  au maharage
• Robo sahani: Ndizi, ugali au wali kidogo
• Tunda: kipande kidogo cha chungwa, Tufaa au Tango

Angalizo: maelezo haya ni mfano tu wa muongozo wa sahani kwa mgonjwa wa Kisukari kwenye wakati milo mikubwa miwili 

💬 MAONI 0

Bado hakuna maoni.
Kuwa wa kwanza kusema kitu.

— ANZA MAZUNGUMZO —