🏥
Kwa mgonjwa wa kisukari, inashauriwa kula milo 3 mikuu na vitafunwa 1–2 kwa siku. Katika kila mlo, chagua kimojawapo kati ya vyakula vilivyotajwa.
- Kiamsha kinywa (Breakfast)
Chagua kimojawapo kati ya:
- Uji wa ulezi au mtama, Chai ya viungo na: Kipande cha mkate wa brown, Yai la kuchemsha, Mtindi usio na sukari, karanga n.k
- Chakula cha mchana (Lunch)
Chagua kimojawapo kati ya wanga:
- Ugali wa dona, Wali wa kahawia, Ndizi za kupika, Viazi vitamu
Kisha chagua kimojawapo kati ya protini:
- Samaki, Kipande kidogo cha kuku, Maharage, Dengu
Na mboga:
- Mchicha, Kabichi, Matembele, Kisamvu, Biringany, n.k
- Chakula cha jioni (Dinner)
kama ilivyo chakula cha mchana isipokua punguza kiasi
- Vitafunwa (Snacks) kati ya milo
Chagua kimojawapo kati ya: Tufaha, Tango, Karanga chache, biskuti zisizo na sukari, n.k - N. B: Kuacha kula sio Tiba ya Kisukari
MAONI
0
Bado hakuna maoni.
Kuwa wa kwanza kusema kitu.