BONGOSOUL
Tupo Kwenye Kila Trend · Tanzania 🇹🇿
EST. 2024 🇹🇿
Wellness & Lifestyle

Fahamu kuhusu ueneaji wa Shinikizo la Damu (Hypertension) Kulingana na Shirika la Afya Duniani (WHO)

Inakadiriwa kuwa watu wazima bilioni 1.4 wenye umri wa miaka 30–79

Fahamu kuhusu ueneaji wa Shinikizo la Damu (Hypertension) Kulingana na Shirika la Afya Duniani (WHO)

Inakadiriwa kuwa watu wazima bilioni 1.4 wenye umri wa miaka 30–79 duniani walikuwa na shinikizo la damu (hypertension) mwaka 2024; hii inawakilisha takribani asilimia 33 ya watu katika kundi hili la umri.

Theluthi mbili (2/3) ya watu wazima wenye umri wa miaka 30–79 walio na shinikizo la damu wanaishi katika nchi za kipato cha chini na cha kati.

Inakadiriwa kuwa watu wazima milioni 600 wenye shinikizo la damu (asilimia 44) hawajui kuwa wana ugonjwa huo.

Takribani watu wazima milioni 630 wenye shinikizo la damu (asilimia 44) wamegunduliwa na wanapata matibabu.

Takribani watu wazima milioni 320 wenye shinikizo la damu (asilimia 23) ugonjwa wao umedhibitiwa vizuri.

Shinikizo la damu ni moja ya sababu kuu za vifo vya mapema duniani.

Moja ya malengo ya kimataifa ya kupunguza magonjwa yasiyoambukiza ni kupunguza kiwango cha shinikizo la damu lisilodhibitiwa kwa asilimia 25 kati ya mwaka 2010 na 2025.

💬 MAONI 0

Bado hakuna maoni.
Kuwa wa kwanza kusema kitu.

— ANZA MAZUNGUMZO —